Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 17:08

Wanajeshi wavunja kambi ya waandamanaji Sri Lanka


Walinzi wakiwa nje ya jengo la bunge mjini Colombo awali
Walinzi wakiwa nje ya jengo la bunge mjini Colombo awali

Mamia ya wanajeshi wa Sri Lanka pamoja na polisi mapema Ijumaa wamevamia kambi moja ya waandamanaji wanaoipinga serikali kwenye mji mkuu wa Colombo, wakati wakiharibu mahema ya wanaharakati wanaosemekana kutokuwa na silaha.

Maafisa hao wamefika kwenye kambi hiyo wakati waandamanaji wakizingira majengo ya ofisi za rais, saa chache kabla ya wakati waliokuwa wamepanga kuondoka. Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, waandamanaji hao walikuwa wameahidi kuondoka eneo hilo baadaye Ijumaa, baada ya baraza jipya la mawaziri kutangazwa na rais mpya aliyeapishwa Ranil Wickremesinghe.

Walioshuhudia wanasema kwamba waliona wanajeshi wakizunguka ofisi hizo zilizopo karibu na bahari, wakati wakivunja vibanda vya muda, vilivyowekwa na maelfu ya waandamanaji tangu Aprili. Maafisa walitumia vyombo vya kupasa sauti kuomba watu waliokusanyika waondoke kwenye eneo hilo.

Waandamanaji wa kampeni ya GoHomeGota, waliokuwa wakishinikiza kuondoka kwa rais Gotabaya Rajapaksa, wamekuwa wakikita kambi kwenye makazi ya rais, kabla ya kumlazimisha kutoroka Julai 9. Baada yake kuondoka, Wickremesighe alishika usukani wakati huo akiwa waziri mkuu.

XS
SM
MD
LG