Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 08:30

Wana usalama wa  serikali wavamia makazi ya rais nchini Peru


Waendesha mashtaka wakiondoka katika Ikulu ya rais kama sehemu ya uchunguzi dhidi ya Rais Boluarte, mjini Lima
Waendesha mashtaka wakiondoka katika Ikulu ya rais kama sehemu ya uchunguzi dhidi ya Rais Boluarte, mjini Lima

Picha za televisheni zilisambaa huko Peru Ijumaa jioni zikionyesha wana usalama wa  serikali kutoka kwenye  timu ya wapelelezi wakivamia makazi ya rais kwa kutumia nyundo katika uvamizi ulioidhinishwa na mahakama kwa ombi la ofisi ya mwanasheria mkuu.

Dina Boluarte anafanyiwa uchunguzi wa awali kwa kuwa na mkusanyo wa saa za kifahari ambao haujatajwa tangu aingie madarakani Julai 2021 kama makamu wa rais na waziri wa Ushirikishwaji wa Jamii, na kisha kama rais Desemba 2022.

Hapo awali, alidai umiliki wa angalau Rolex moja kama milki ya muda mrefu iliyopatikana kibinafsi tangu akiwa na umri wa miaka 18, akitaka vyombo vya habari kutojishughulisha na masuala ya kibinafsi.

Machafuko ya kisiasa si jambo geni nchini Peru, ambayo imeshuhudia marais sita katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Lakini wengi wanaona kauli za hivi karibuni za Boluarte kuwa zinapingana na ahadi yake ya awali ya kuzungumza ukweli na waendesha mashtaka, na hivyo kuzidisha mzozo wa kisiasa unaotokana na umiliki wake usioelezeka wa saa za gharama kubwa za Rolex.

Forum

XS
SM
MD
LG