Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Februari 19, 2025 Local time: 02:49

Wakulima wa Poland waandamana Jumapili kulalamikia sheria za EU


Wakulima wa Poland wakiwa wamefunga barabara kuu kuelekea Ujerumani, kulalamikia EU.
Wakulima wa Poland wakiwa wamefunga barabara kuu kuelekea Ujerumani, kulalamikia EU.

Wakulima wa Poland Jumapili wamefunga barabara muhimu inayoelekea Ujerumani, yakiwa maandamano ya karibuni zaidi ya kulalamikia sera mpya za Umoja wa Ulaya pamoja na kodi.

Wakulima kote Ulaya kwa wiki kadhaa sasa wamekuwa wakiandamana kupinga kile wanachosema ni kanuni kandamizi za kimazingira, ushindani kutokana na bidhaa za gharama ya chini kutoka nje ya EU, pamoja na mapato ya chini.

Barabara iliofungwa na wakulima hao ni ile ya A2 karibu na mji wa Slubice, ulioko mashariki mwa Poland, karibu na mpaka wa Ujerumani. Mwanzoni, walipanga kufunga barabara hiyo kwa siku 25, lakini walipunguza muda huo baada ya mashauriano na wawakilishi wa utawala wa kieneo, wafanyabiashara pamoja na wasafirishaji bidhaa.

Mmoja wa viongozi wa wakulima hao Dariusz Wrobel, alisema kwamba wamekubali kufungua barabara hiyo ifikapo Jumatatu. Hata hivyo, hilo litategemea masuala yasioweza kutabirika, ameambia shirika la habari la AFP. Mawaziri wa Kilimo kutoka mataifa wanachama wa EU, wamepangiwa kukutana Jumatatu mjini Brussels.

Forum

XS
SM
MD
LG