Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Mei 02, 2024 Local time: 06:42

Wakenya Kipchoge na Cherono washinda Berlin Marathon


Manariadha wa Kenya Eliud Kipchoge ambaye alishinda mbio za Berlin Marathon, Septemba 24 2017.
Manariadha wa Kenya Eliud Kipchoge ambaye alishinda mbio za Berlin Marathon, Septemba 24 2017.

Bingwa wa Olympic katika mbio za marathon, Eliud Kipchoge, Jumapili alishinda mbio za Berlin Marathon dhidi ya mpinzani wake wa karibu Guye Adola kutoka Ethiopia.

Kipchoge, ambaye ni raia wa Kenya, alishinda mbio hizo kwa kukimbia kwa muda wa saa mbili, dakika tatu na sekunde 32.

Hata hivyo, hakuweza kufikia kiwango cha ubingwa wa kimataifa kwa sekunde 35 kutokana na hali ya unyevu uliosababishwa na mvua.

Mwanariadha huyo alinukuliwa na shirika la habari la Associated Press, AP, akisema kuwa mbio hizo zilikuwa ngumu kuliko mbio zingine zote za Marathon ambazo amewahi kushiriki.

Adola alimaliza mbio hizo sekunde 14 nyuma ya Kipchoge. Kwa upande wa wanawake, Mkenya Gladys Cherono alishinda mbio hizo kwa kukimbia kwa muda was aa mbili, dakika 20 na sekunde 23.

XS
SM
MD
LG