Maelfu ya watu wanakimbia Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo wakihofia kwamba matokeo ya uchaguzi yatakayotangazwa jumanne yanaweza kupelekea kulipuka ghasia .
Polisi katika nchi jirani ya Jamhuri ya Congo wanasema watu wapatao 3,000 wamewasili katika mji mkuu Brazaville tangu Desemba 2.
Maafisa wanasema wengi wa waliowasili wanatoka mji mkuu wa DRC Kinshasa ambao wanaishi kwenye eneo la mto Congo kutoka Brazaville ambapo hali ni ya mvutano.