Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 18, 2025 Local time: 13:11

Waislamu kutoka kote ulimwenguni wajumuika kwenye ibada muhimu katika mlima Arafat Saudi Arabia


Saudi Arabia Hajj
Saudi Arabia Hajj

Kufuatia nyayo za manabii  Waislamu kutoka kote ulimwenguni walijumuika Jumamosi kwenye mlima mtakatifu huko Saudi Arabia kwa ibada ya mchana na tafakuri.

Ibada katika Mlima Arafat, unaojulikana kama kilima cha huruma, inachukuliwa kuwa kilele cha Hija. Mara nyingi ni jambo la kukumbukwa zaidi kwa mahujaji, wanaosimama bega kwa bega, mguu kwa mguu, wakimwomba Mwenyezi Mungu huruma, baraka, mafanikio na afya njema. Mlima huo uko kiasi cha kilomita 20 kusini mashariki mwa Makka.

Maelfu ya mahujaji walitembea hadi mlimani wakati wa giza la alfajiri. Kwenye miteremko ya kilima chenye mawe na eneo linalozunguka, wengi waliinua mikono yao juu katika ibada huku machozi yakiwatoka.

Forum

XS
SM
MD
LG