Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 05:40

Wahodhi watishia kuanza oparesheni zao


Kiongozi wa waasi wa Kihouthi wa Yemen, Ijuma amesema kundi hilo litarudia operesheni zake za kijeshi dhidi ya Israel, endapo Israel haitaondoa kizuizi cha misaada cha Gaza ndani ya siku nne.

Jambo linaloashiria uwezekano wa kuongezeka ghasia za Wahouthi baada ya mashambulizi yao kutoweka mwezi Januari kufuatia kusitishwa kwa mapigano katika eneo hilo.

Kundi hilo linaloungwa mkono na Iran lilianzisha mashambulizi zaidi ya 100 yakilenga meli kuanzia Novemba 2023, kwa kutoa mshikamano kwa Wapalestina kutokana na vita vya Israel na Hamas, ambayo imetangazwa na Marekani kuwa kundi la kigaidi, huko Gaza.

Katika kipindi hicho, lilizamisha meli mbili, kukamata nyingine na kuua takriban mabaharia wanne, mashambulizi yaliyo sumbua usafiri wa meli ulimwenguni, na kulazimisha kampuni kutumia safari ndefu na za gharama kuzunguka kusini mwa Afrika.

Forum

XS
SM
MD
LG