Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Mei 02, 2024 Local time: 08:01

Wahandisi waangazia kazi ya kusafirisha mabaki ya Daraja la Francis Scott Baltimore


Don Bryant wa Kituo cha Kimataifa cha Wasafiri wa Baharini akiwapeleka wafanyakazi wa melini katika moja ya meli zilizokwama katika Bandari ya Baltimore kufuatia kuporomoka kwa Daraja kuu la Francis Scott, huko Baltimore, Maryland, Marekani, Machi. 29, 2024. REUTERS.
Don Bryant wa Kituo cha Kimataifa cha Wasafiri wa Baharini akiwapeleka wafanyakazi wa melini katika moja ya meli zilizokwama katika Bandari ya Baltimore kufuatia kuporomoka kwa Daraja kuu la Francis Scott, huko Baltimore, Maryland, Marekani, Machi. 29, 2024. REUTERS.

Vikundi vya wahandisi sasa vimeangazia kazi kubwa ya kusafirisha mabaki yaliyovunjika ya Daraja kuwa la Francis Scott kutoka Mto Patapsco huko Maryland, hatua ya kwanza ya kufungua tena Bandari ya Baltimore na kuopoa miili ya wafanyakazi wanne ambao bado hawajapitakana na wanaodhaniwa kuwa wamekufa.

Meli kubwa ya mizigo iliangusha daraja hilo Jumanne baada ya kugonga mojawapo ya nguzo zake kuu. Wataalam wanajaribu kufikiria jinsi ya “kukata daraja hilo katika vipande sawa vya ukubwa ambavyo tunaweza kuinua,” Kamanda mkuu wa kikosi cha walinzi wa pwani Admirali Shannon Gilreath alisema Ijumaa katika mkutano na wanahabari. Zana zinazohitajika zimeanza kutumika.

Ni pamoja na Kreni saba za kuinua mizigo, za kuelea majini, mojawapo ikiwa ni kubwa zaidi kwa kanda nzima ya mashariki mwa Marekani, yenye uwezo wa kuinua tani 1,000, boti 10 za kuvuta, mashua tisa, boti nane za kubeba mizigo, na boti tano za Walinzi wa Pwani.

Forum

XS
SM
MD
LG