Miili ya wahamiaji hao wawili ilionekana juu ya majii baada ya boti lao kuzama, MAP imeripoti bila kutoa maelezo zaidi.
Katika tukio jingine, maafisa wa Morocco waliwakamata wahamiaji 236 katika operesheni za msako Ijumaa na Jumamosi katika mkoa wa kusini wa Tarfaya na mji wa Laayoune, mji mkuu wa eneo lenye ugomvi la Western Sahara.
Inaarifiwa kuwa wahamiaji hao walikuwa wanataka kuvuka kuelekea visiwa vya Spain vya Canary.
Mkoa wa Tarfaya unapatikana umbali wa kilomita 100 na visiwa vya Canary na kimekua kituo kikuu cha usafiri kwa wahamiaji wanaotarajia kufika Ulaya.