Umoja wa Mataifa unataka kuwepo na utulivu katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo baada ya waangalizi wa Ulaya kutangaza matatizo katika upigaji kura mapema wiki hii. Mkuu wa tume ya Umoja wa Mataifa Roger Meece alisema malalamiko yoyote lazima yatangazwe kupitia njia za amani. Ripoti ya awali ya Umoja wa Ulaya inasema waangalizi wa uchaguzi walisema wameona masanduku yakiwa yameshajazwa kura na kwingine hayakuwepo ambapo baadhi ya watu walirudishwa na kuzuiwa kupiga kura.