Maelfu ya waandamanaji waliruka vizuizi vya usalama, wakapanda juu ya mapaa, wakavunja madirisha na kuvamia majengo yote matatu, ambayo yameunganishwa na eneo kubwa la Three Powers Square mjini Brasilia.
Wengine waliomba uingiliaji kati wa jeshi ili kumrejesha madarakani Bolsonaro wa mrengo mkali wa kulia na kumuondoa Lula katika urais.
Kituo cha televisheni cha Globo News kilionyesha waandamanaji wakizurura ndani ya ikulu, wengi wao wakiwa wamevalia rangi za kijani na manjano za bendera ya taifa ambazo pia zimeashiria vuguvugu la kihafidhina la taifa hilo lililoanzishwa na Bolsonaro.
Rais huyo wa zamani ambaye alisafiri kuja Marekani kabla ya kuapishwa kwa Lula, alikuwa hajasema chochote kuhusu matukio ya Jumapili.
Matukio hayo yalikumbusha shambulio la Januari 6, 2021 kwenye Bunge la Marekani lililofanywa na wafuasi wa rais wa wakati huo Donald Trump.