Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 04, 2024 Local time: 05:27

Waasi wa Red Tabara wauwa wanajeshi kwenye shambulizi la Burundi


Wanajeshi wa Burundi wakikamata wafuasi wa Red Tabara. Picha ya maktaba.
Wanajeshi wa Burundi wakikamata wafuasi wa Red Tabara. Picha ya maktaba.

Msemaji wa serikali ya Burundi amesema Jumatatu kwamba watu wenye silaha kutoka kundi la waasi la Red Tabara wameua watu 9 na kujeruhi wengine kwenye mashambulizi ya usiku kucha magharibi mwa mwa nchi karibu na mpaka wake na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Red Tabara limekuwa likipigana na serikali ya Burundi kutoka kwenye vituo vyake ndani ya Congo tangu 2015. Kupitia ujumbe wa X iliojulikana kama Twitter, Red Tabara limesema kwamba limeshambulia vituo viwili vya kijeshi vya Burundi Jumapili usiku, wakati likiteka silaha pamoja na risasi, na kwamba wanajeshi 6 waliuwawa.

Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye mwishoni mwa Desemba alisema kuwa Rwanda alikuwa ikitoa hifadhi pamoja na mafunzo kwa kundi hilo, kufuatia shambulizi lingine ambalo serikali yake ilisema lilikuwa takriban watu 20. Baadaye Burundi ilifunga mpaka wake na Rwanda, ambayo ilikanusha madai ya Ndayashimiye

Forum

XS
SM
MD
LG