Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Mei 09, 2024 Local time: 02:04

Waasi wa ADF waua watu 15 mashariki mwa DRC


Ramani ya DRC
Ramani ya DRC

Waasi wanaodhaniwa kuwa wa kundi la ADF lenye uhusiano na kundi la kigaidi la Islamic State wameua watu 15 Jumapili katika msururu wa mashambulizi kwenye vijiji tofauti huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, maafisa wa eneo hilo wamesema.

Mauaji hayo yanajiri wiki moja baada ya shambulio kama hilo ambalo lillisababisha vifo vya zaidi ya watu 20.

“Kulikuwa na mashambulizi ya wakati mmoja kati ya saa kumi na saa kumi na moja alfajiri kwenye vijiji vitatu,” afisa wa eneo hilo Dieudonne Malangai amesema.

Malangai ameiambia AFP kwamba “waligundua miili 7 katika kijiji cha Manyala, na huko Ofay kulikuwa miili nane, ikiwemo saba ya wanawake.”

Chanzo kutoka mashirika ya misaada kimethibitisha vifo vya watu saba huko Manyala na vingine nane huko Ofay.

“Waasi hao wa ADF walishambulia pia kijiji cha Bandibese lakini walitimka baada ya wanajeshi kuingilia kati na hakuna raia waliouawa katika kijiji hicho,” amesema Malangai baada ya mashambulizi hayo kwenye vijiji vya mkoa wa Ituri unaopakana na Uganda.

Wapiganaji wa ADF walishtumiwa pia kwa mashambulizi ya wiki iliyopita katika mkoa jirani wa Kivu Kaskazini ambayo yalisababisha vifo vya watu 23. Katika mkoa huo huo watu 14 waliuawa katika shambulizi la bomu kwenye kanisa la Kipentekoti.

XS
SM
MD
LG