Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:16

Waandamanaji wataka rais mteule wa Brazil asichukuwe madaraka


Wafuasi wa rais wa Brazil, Jair Bolsonaro, wakipiga saluti wakati wimbo wa taifa ukiimbwa katika maandamano nje ya makao makuu ya jeshi mjini Brasilia, Brazil, Novemba 15, 2022.
Wafuasi wa rais wa Brazil, Jair Bolsonaro, wakipiga saluti wakati wimbo wa taifa ukiimbwa katika maandamano nje ya makao makuu ya jeshi mjini Brasilia, Brazil, Novemba 15, 2022.

Maelfu ya raia wa Brazil walikusanyika nje ya kambi za jeshi jijini Rio de Janeiro, Brasilia na miji mingine Jumanne yakitaka jeshi kuingilia kati kuzuia rais mteule wa mrengo wa kushoto wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva kuchukuwa madaraka mwakani.

Waandamanaji walibeba bendera ya Brazil na kuimba wimbo wa taifa katika sikukuu ya kibenki.

Wafuasi wa rais anaye ondoka madarakani Jair Bolsonaro, wameshutumu kufanyika udanganyifu katika mifumo ya uchaguzi ambayo imekuwa ikitumika toka mwaka 1996.

Bolsonaro vilevile amekuwa akitoa madai hayo licha ya kutoa uthibitisho wowote.

Wizara ya ulinzi ya Brasil, hata hivyo imetoa ripoti kupinga madai hayo ya uchaguzi kuwa na udanganyifu huku waangalizi wa kimataifa pia wakithibitisha uhalali wa uchaguzi.

Lula pia alikuwa rais wa Brazil kuanzia mwaka 2003 mpaka 2010 na kuondoka madarakani akiwa anakubalika kwa kiwango kikubwa.

XS
SM
MD
LG