Maelfu ya waandamanaji walivamia makazi hayo mawili Jumamosi. Walivamia nyumba ya Rais Rajapaksa na kuchoma makazi ya waziri mkuu Ranil Wickremesinghe wakati kukiwa hasira ya umma juu ya mzozo wa kiuchumi uliodumu kwa miezi kadhaa.
Kufuatia hayo, Rajapaksa na waziri mkuu walikubali kujiuzulu huku rais akimuelezea spika wa bunge kuwa ataondoka madarakani Julai 13 ili kuhakikisha kipindi cha mpito kinafanyika kwa usalama.
Hata hivyo, waandamanaji wanataka viongozi hao kujiuzulu mara moja.
Rais Rajapaksa alipelekwa na wanajeshi mahali salama, sehemu ambayo haikutangazwa kabla ya maandamano hayo makubwa.
Akilaumiwa sana kwa kuzorota kwa uchumi, rais alikuwa chini ya shinikizo la umma kujiuzulu kwa miezi kadhaa sasa.