Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 11:17

Waandamanaji Sri Lanka wanataka kaimu rais naye ang'atuke haraka iwezekanavyo


Waandamanaji, baadhi yao wakiwa wamebeba bendera ya taifa, wakiwa katika ofisi za waziri mkuu Ranil Wickremesinghe. wanamtaka Ranil, ambaye sasa ni kaimu rais, waondoke madarakani. PICHA: AP
Waandamanaji, baadhi yao wakiwa wamebeba bendera ya taifa, wakiwa katika ofisi za waziri mkuu Ranil Wickremesinghe. wanamtaka Ranil, ambaye sasa ni kaimu rais, waondoke madarakani. PICHA: AP

Waandamanaji wamekusanyika katika kituo cha treni mjini Colombo nchini Sri Lanka kutaka kaimu rais Ranil Wickremesinghe aondoke madarakani.

Ranil aliteuliwa kuwa rais wa mda wa Sri Lanka baada ya Gotabaya Rajapaska kukimbilia nchi hiyo na kwenda uhamishoni ambapo alitangaza kujiuzulu kufuatia maandamano ya miezi kadhaa.

Maandamano yamekuwa yakiendelea Sri Lanka baada ya uchumi wa nchi hiyo kuanguka.

Kaimu rais Ranil, alitangaza hali ya dharura na kumpa mamlaka makubwa ya kuongoza nchi hiyo licha ya maandamano kuongezeka kutaka ajiuzulu.

Bunge la Sri Lanka linatarajiwa kumchagua rais mpya katika mda wa siku mbili.

Waandamanaji wamesema kwamba tangazo la hali ya dharura halitawazuia kuendelea kutaka kuundwa kwa serikali mpya.

Maandamano hayo yanaingia siku ya 100, huku Zaidi ya watu milioni 22 wakikabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula, mafuta na dawa tangu mwishoni mwa mwaka uliopita.

XS
SM
MD
LG