Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 10:59

Vyama vya upinzani nchini Guinea, vyakaidi marufuku ya kufanya maandamano


Kiongozi wa utawala wa kijeshi nchini Guinea Kanali Mamady Doumbouya, akisalimia majaji wa mahakama katika hafla ya kula kiapo kama rais wa nchi, October 1, 2021. Picha ya AFP
Kiongozi wa utawala wa kijeshi nchini Guinea Kanali Mamady Doumbouya, akisalimia majaji wa mahakama katika hafla ya kula kiapo kama rais wa nchi, October 1, 2021. Picha ya AFP

Vyama vikuu vya upinzani nchini Guinea Jumatatu vimeapa kukaidi marufuku ya kutofanya maandamano iliyowekwa na utawala wa kijeshi, hatua ambayo inaashiria uhusiano mbaya kati ya vyama hivyo na jeshi katika siku zijazo.

Muungano huo wa vyama vya upinzani unaojulikana kama G58 uliungana na chama cha rais wa zamani Alpha Conde RPG, kutangaza nia yao ya kupinga marufuku hiyo na kushtumu “ubabe” wa kiongozi wa kijeshi Kanali Mamady Doumbouya katika taarifa kwa vyombo vya habari.

Katika nchi ambayo imezoea ghasia za kisiasa, vyama hivyo vimeonya kwamba viongozi wa kijeshi “watawajibika pekee yao kwa kuzorotesha” hali ya kijamii katika siku zijazo.

Wakikerwa na ukandamizaji, umaskini na ufisadi chini ya utawala wa Conde, wengi waliukaribisha uongozi wa kijeshi uliponyakua madaraka kutoka kwake mwezi Septemba mwaka jana.

Lakini malalamiko yanaongezeka miongoni mwa vyama vya siasa.

Kundi la G58 na chama cha RPG wamesema katika taarifa yao kwamba hawakubaliani kamwe na marufuku mpya ya maandamano iliyotangazwa siku ya Ijumaa, na wameazimia “kutetea utawala wa sheria”, na katika hali hii kutetea haki ya kuandamana.

Wamesema wataunda kamati ya kuandaa “maandamano ya amani siku zijazo.”

XS
SM
MD
LG