Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 15:08

Vitalu vya mafuta vimewaka moto Russia


Ndege isiyokuwa na rubani iliyoharibiwa imeangukia vitalu vya mafuta katika Oryol
Ndege isiyokuwa na rubani iliyoharibiwa imeangukia vitalu vya mafuta katika Oryol

Maafisa wa Russia wamesema leo jumanne kwamba mabaki ya ndege isiyokuwa na rubani iliyoharibiwa, yameangukia vitalu vya mafuta katika mji wa Smolensk na kusababisha moto.

Wizara ya ulinzi ya Russia imesema kwamba iliangusha ndege zisizokuwa na rubani 68 zilizorushwa na Ukraine, usiku wa kuamkia leo, ikiwa ni pamoja na 10 zilizopita juu ya mji wa Smolensk.

Makombora mengine yamezuiliwa katika miji ya Bryansk, Crimea, Krasnodar, Tver, Rostov, Kursk na Kaluga.

Hakuna ripoti zaidi za uharibifu au vifo.

Wakati huo huo, mfumo wa ulinzi wa Ukraine umezuia makombora yaliyorushwa na Russia katika mji wa Kyiv, leo Jumanne.

Kiongozi wa kijeshi katika mji wa Kyiv, Serhii Popko, amesema mabaki kutoka kwa makombora yaliyozuiliwa yameangukia ajengo lakini hakuna uharibifu ulitokea.

Forum

XS
SM
MD
LG