Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 27, 2025 Local time: 03:19

Visa vya raia kupiga wenzao risasi vimeongezeka Marekani


Rais wa Marekani Joe Biden na mke wake Jill Biden wwakitoa heshima kwa wahanga wa mauaji ya risasi New York May 17 2022 PICHA: Reuters
Rais wa Marekani Joe Biden na mke wake Jill Biden wwakitoa heshima kwa wahanga wa mauaji ya risasi New York May 17 2022 PICHA: Reuters

Idhara ya upelelezi wa jinai Marekani FBI imesema kwamba visa vya watu kupiga wenzao risasi nchini Marekani viliongezeka kwa zaidi ya asilimia 50 mnamo mwaka 2021, ikilinganishwa na mwaka 2020.

Visa 61 viliripotiwa, ikiwa ni mara mbili ya ilivyorekodiwa miaka mitano iliyopita.

Watu 103 waliuawa na 140 kujeruhiwa mwaka 2021. Hesabu hiyo haijumulishi watu waliokuwa wakitekeleza mashambulizi hayo.

Ripoti hiyo imetolewa siku 9 baada ya kijana mwenye umri wa miaka 19 kuwaua watu 10 na kujeruhi wengine watatu katika jamii inayokaliwa sana na watu weusi, katika mtaa wa Buffalo, mjini New York.

FBI inachunguza kisa hicho kama cha uhalifu wa chuki na kilichochochewa na ubaguzi wa rangi.

XS
SM
MD
LG