Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 09, 2025 Local time: 21:19

Viongozi wa kijeshi wa Niger wapunguza bajeti ya nchi kutokana na vikwazo vya kimataifa


Kiongozi wa kijeshi wa Niger, Jenerali Abdourahmane Tiani
Kiongozi wa kijeshi wa Niger, Jenerali Abdourahmane Tiani

Viongozi wa kijeshi wa Niger wametangaza kupunguzwa kwa kiasi kikubwa kwa bejeti ya mwaka huu, wakitaja vikwazo vya kimataifa vilivyowekewa taifa hilo tangu wachukuwe madaraka katika mapinduzi zaidi ya miezi miwili iliyopita.

Nchi hiyo ambayo ni moja kati ya nchi maskini duniani, inategemea sana msaada wa kigeni kusaidia wanainchi wake milioni 25, lakini msaada huo ulipungua tangu wanajeshi walipomuondoa madarakani rais Mohamed Bazoum tarehe 26 Julai.

“Niger inakabiliwa na vikazo vikali vilivyowekwa na mashirika ya kimataifa na kikanda. Vilisababisha mapato kupungua sana,” viongozi wa kijeshi walisema kwenye televisheni ya taifa Ijumaa jioni.

Bajeti ya mwaka wa 2023 ilipunguzwa kwa asilimia 40 hadi dola bilioni 3.2, taarifa hiyo imesema.

Forum

XS
SM
MD
LG