Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 21, 2025 Local time: 20:20

Vikosi vya Russia na Ukraine vyaendelea kushambuliana


Nyumba binafsi za watu zilizoharibiwa na shambulizi la kombora la Russia katika mji wa Novomoskovsk, near Kryvyi Rih, Ukraine, Monday, Jan. 8, 2024. (Ukrainian Emergency Service via AP).
Nyumba binafsi za watu zilizoharibiwa na shambulizi la kombora la Russia katika mji wa Novomoskovsk, near Kryvyi Rih, Ukraine, Monday, Jan. 8, 2024. (Ukrainian Emergency Service via AP).

Vikosi vya Russia na Ukraine vimeendelea kushambuliana katika mapigano yaliyoendelea Jumatatu ambapo kila mmoja amedai kulenga maeneo ya kijeshi ambayo ni pamoja na vituo vya ulinzi na maghala ya silaha.

Wizara ya Ulinzi ya Russia Jumatatu ilitoa ripoti ya mapigano ikisema kuwa jeshi la Russia lilivamia majengo ya ulinzi ya Ukraine kwa kutumia silaha zake za kulenga shabaha, ili kurudisha nyuma mashambulizi ya kijeshi ya Ukraine.

Operesheni hii iko katika maeneo mbalimbali ikiwemo Donetsk, Kupiansk na Kherson na pia kuvamia kituo chake cha udhibiti cha mfumo wa ndege zisizo na rubani UAV, ghala la silaha na malengo mengine.

Jeshi la anga la Russia limesema pia lilizuia mashambulizi ya roketi kadhaa na ndege zisizokuwa na rubani za jeshi la Ukraine.

Siku hiyo hiyo, mkuu wa majeshi ya Ukraine pia alitoa taarifa juu ya maendeleo ya mapigano akisema kuwa katika saa 24 zilizopita jeshi la ukraine limeendelea kupigana katika maeneo mbalimbali na jeshi la Russia katika ukingo wa mto Dnieper na maeneo mengine.

Chanzo cha habari hii ni shirika la habari la AP.

Forum

XS
SM
MD
LG