Kwa mujibu wa shirika la habari la AP, Ramaphosa amesema kwamba, " Huenda tusifahamu hasa kilichotokea, lakini tunachofahamu ni kwamba sheria ilivunjwa usiku huo, na labda mara kadhaa hapo kabla." Mazishi hayo yanasemekana kuhudhuriwa na zaidi ya waombolezaji 1,000 kwenye mji wa East London wakati majeneza yakipangwa katika mistari miwili.
Ramaphosa amehudhuria mazishi hayo wakati taifa lake linapokabiliana na changamoto kadhaa zikiwemo kukatika kwa huduma za umeme, madai ya ufisadi pamoja na uchunguzi unaoendelea wa fedha nyingi zilizopatikana zikiwa zimefichwa kwenye nyumba moja kwenye shamba lake.