Miaka miwili baada ya kutekwa wasichana zaidi ya 200 kaskazini mwa Nigeria na kundi la Boko Haram, video mpya inayoonyesha wasichana hao waliopotea ikiwa ni miezi minne tu iliyopita imewapa wazazi matumaini kwamba watoto wao bado wako hai.
Mpaka sasa kumekuwa hakuna habari yeyote juu ya wasichana hao 219 waliotekwa na Boko Haram 2014 kutoka shule moja katika mji wa Chibok jambo ambalo lilipelekea shutuma ya ulimwengu mzima, maandamano ya mitaani nchini Nigeria na watu wakijitolea kusaidia kuwatafuta kutoka nchi washirika.
Video mpya iliyoonekana Jumatano ambayo inaonyesha wasichana 15 kati yao na huenda imechukuliwa mwezi Desemba, hiyo ni alama ya kwanza ya waliotekwa tangu walipoonekana kwenye video ya Boko Haram ya propaganda muda mfupi baada ya kutekwa.