Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Machi 26, 2025 Local time: 21:27

Vatican yasema Papa anaendelea vyema


Maafisa wa Vatican Jumamosi wamesema Papa Francis alipumzika kwa amani baada ya kupata shida ya kupumua Ijumaa.

“Papa alikuwa na usiku wa amani na anapumzika,” Vatican imesema katika taarifa. Papa Francis alipata shida Ijumaa wakati akiwa katika hospitali ya Gemelli ya Roma, ambapo amelazwa kwa wiki mbili zilizopita.

Vatican imesema “tukio la pekee la kupumua” lilisababisha Papa mwenye umri wa miaka 88 kuvuta matapishi yake ambayo yalihitaji uingizaji hewa kwa mitambo.

Papa Francis alikuwa na fahamu wakati wa kipindi chote na aliweza kushirikiana na kushiriki nyanja mbalimbali za matibabu yake.

Vatican imesema Papa bado anafahamu zote na mwenye mwelekeo mzuri.

Habari za matatizo ya Ijumaa zinafuatia siku tatu za ripoti za kuboreka kwa hali ya afya ya Papa Francis.

Forum

XS
SM
MD
LG