Mamia ya watu waliobeba bendera nyekundu za Uturuki nyingine zikiwa na urefu wa mita 10 waliandamana jana jumapili kuelekea uwanja wa Joseph eneo la kihistoria la Vienna.
Waandamanaji hao walikuwa wakipinga mashambulizi ya wiki iliyopita katika uwanja wa ndege wa Instanbul uliouwa watu 45 na karibu 250 kujeruhiwa, wanashutumu sehemu ya serikali ya Austria inayounga mkono wanamgambo wa chama cha PKK -Kurdistan Workers Party ambao wanajulikana kama magaidi katika nchi zote za Austria na Uturuki.
“Serikali ya Austria inabidi iweke msimamo wake dhidi yao alisema Metlhem mwenye umri wa miaka 27” wanaruhusu itokee hapa”.
“Kama wapo kwenye wilaya yeyote lazima waondolewe aliongeza Mustafa Koca mwanafunzi wa mawasiliano ya kompyuta mwenye umri wa miaka 19.