Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 22:41

Uturuki yafikiriwa kuwa mwanachama wa EU


Waziri wa Umoja huo kutoka Uturuki, Omer Celik, na waziri wengine
Waziri wa Umoja huo kutoka Uturuki, Omer Celik, na waziri wengine

Ukurasa mpya umefunguliwa katika juhudi za Uturuki kujiunga na Umoja wa Ulaya huku mashauriano kuhusu kuchangia bajeti yakianza mjini Brussels.

Sura ya 33 inayohusiana na maswala ya kifedha na bajeti imefunguliwa mapema leo.

Uturuki lazima itimize kurasa 35 za uanachama wa Ulaya lakini kurasa tano bado zimezuiliwa kutokana na Ankara kutotambua Cyprus kama taifa.

Hatua ya Ankara ya kujiunga na Umoja wa Ulaya imekuja wiki moja tu baada ya Uingereza kuamua kujitoa kwenye muungano huo jambo ambalo Waziri wa Umoja huo kutoka Uturuki, Omer Celik, amesema litaimarisha nafasi ya nchi yake hata zaidi kwenye muungano huo.

Watu wengi kutoka Ulaya wanapinga uanachama wa Uturuki kutokana na sababu nyingi wengi wakihofia wingi wa waislamu walioko pamoja na hofu kwamba hatua hiyo itafungua milango kwa wahamiaji kuingia mataifa mengine ya Ulaya.

XS
SM
MD
LG