Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 19:39

Uturuki imeendelea kuhoji maombi ya Sweden na Finland kujiunga na NATO


Bendera za Finland, NATO na Sweden wakati wa hafla ya kuthathmini maombi ya Sweden na Finland kujiunga na NATO Mei 18, 2022
Bendera za Finland, NATO na Sweden wakati wa hafla ya kuthathmini maombi ya Sweden na Finland kujiunga na NATO Mei 18, 2022

Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg amesema kwamba muda umefika kwa Finland na Sweden kukubaliwa kuwa wanachama wa muungano huo.

Akizungumza katika kikao na waandishi wa habari mjini Ankara, Uturuki, akiwa na waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Mevlüt Çavuşoğlu, Stoltenberg amesema kwamba suala kubwa sio iwapo nchi hizo mbili zinastahili kuwa wanachama kwa wakati mmoja, lakini maombi yao kuwa wanachama yanastahili kukubaliwa haraka iwezekanavyo.

Çavuşoğlu amesema kwamba Uturuki huenda ikatathmini maombi hayo lakini sio kwa pamoja.

Uturuki na Hungary ndio nchi pekee wanachama wa NATO ambazo hazijarasmisha uanachama wa Finland na Sweden kwenye muungano huo.

Finland na Sweden ziliomba kuwa wanachama wa NATO baada ya Russia kuivamia Ukraine, mwaka uliopita.

Uturuki imesita kuunga mkono ombi la Sweden, ikiishutumu serikali ya Sweden kwa kuwapatia hifadhi wanachama wa makundi ambayo Uturuki inatambua kwamba ni ya kigaidi.

XS
SM
MD
LG