Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 16, 2025 Local time: 18:17

Uturuki: Hesabu ya kura za urais inaendelea, Erdogan anatabiriwa kushinda


Maafisa wa tume ya uchaguzi nchini Uturuki wakihesabu kura za urais katika duru ya pili, mjini Istanbul. May 28, 2023.
Maafisa wa tume ya uchaguzi nchini Uturuki wakihesabu kura za urais katika duru ya pili, mjini Istanbul. May 28, 2023.

Kura zimeanza kuhesabiwa nchini Uturuki, katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais ambapo rais wa sasa Recepp Tayyip Erdogan anatarajiwa kushinda muhula mwingine madarakani.

Erdogan mwenye umri wa miaka 69, ameiongoza Uturuki kwa muda wa miaka 20, alishindwa kupata ushindi wa moja kwa moja katika duru ya kwanza ya uchaguzi mapema mwezi huu.

Kemal Kilicdaroglu, mwenye umri wa miaka 79 ndiye mshindani pekee wa Erdogan.

Uturuki inakabiliwa na matatizo makubwa ya kiuchumi, mfumuko wa bei na athari za tetemeko baya la ardhi lililotokea miezi mitatu iliyopita.

Ushindi wa Erdogan utamuwezesha kuwa kiongozi wa Uturuki kwa mwongo wa tatu.

Wakosoaji wake wanasema kwamba utawala wake umekuwa wa kidikteta.

Ukusanyaji wa maoni unaonyesha kwamba Erdogan ataibuka mshindi. Matokeo rasmi yanatarajiwa katika saa chache zijazo.

Forum

XS
SM
MD
LG