Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:56

Utawala wa Biden utaanza kuwapima Ebola wasafiri wanaoingia  Marekani kutoka Uganda


Fort Worth International Airport: Uwanja wa Ndege Pekee wa Marekani Unaotoa Mipango yote ya Forodha ilioharakishwa kwa wasafiri wa Kimataifa huko Dallas Texas.
Fort Worth International Airport: Uwanja wa Ndege Pekee wa Marekani Unaotoa Mipango yote ya Forodha ilioharakishwa kwa wasafiri wa Kimataifa huko Dallas Texas.

Utawala wa Biden utaanza kuwaelekeza wasafiri wanaoingia  Marekani ambao walikuwa wameenda Uganda ndani ya siku 21 zilizopita hadi kwenye viwanja vya ndege vitano vikuu vya Marekani kuchunguzwa Ebola huku maafisa wa afya ya umma wakituma tahadhari kwa wahudumu wa afya.

Vituo vya Marekani vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) siku ya Alhamisi vilitoa tahadhari kwa wahudumu wa afya ili kuhamasishwa kuhusu mlipuko huo lakini wakasema kwa sasa hakuna kesi zinazoshukiwa au zilizothibitishwa za Ebola nchini Marekani kutoka kwenye Ebola ya Sudan, ambayo ndiyo inayoambukiza nchini Uganda.

Kulingana na Wizara ya Afya ya Uganda takriban watu tisa walifariki kutokana na ugonjwa huo nchini Uganda kufikia Oktoba 3. Maafisa katika taifa hilo la Afrika Mashariki walitangaza kuzuka kwa homa hiyo hatari ya kuvuja damu mnamo Septemba 20. Kuna jumla ya kesi 43, ikiwa ni pamoja na vifo.

Upimaji Marekani ulianza Alhamisi kwenye viwanja vya ndege lakini mahitaji kamili ya uboreshaji yanatarajiwa kuanza kutumika ndani ya wiki moja ijayo, chanzo kiliiambia Reuters.

XS
SM
MD
LG