Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Januari 13, 2025 Local time: 12:46

Utafiti waonyesha zaidi ya watoto 9,000 walifanyiwa unyanyasaji wa kingono katika Kanisa la Kiprotestanti la Ujerumani


Tamasha likifanyika wakati wa ufunguzi wa kongamano la Kanisa la Protestanti la Ujerumani mjini Berlin, Mei 24, 2017.
Tamasha likifanyika wakati wa ufunguzi wa kongamano la Kanisa la Protestanti la Ujerumani mjini Berlin, Mei 24, 2017.

Utafiti kuhusu unyanyasaji wa kingono dhidi ya watoto katika Kanisa la Kiprotestanti la Ujerumani (EKD) umekadiria kuwa idadi ya watoto walioathiriwa inaweza kuwa juu kufikia 9,355.

Utafiti huo uliochapishwa Alhamisi, ulifanya makadirio hayo baada ya kukagua kesi 2,225 za dhulma ya kingono zilizochunguzwa na kubaini wahusika 1,259 tangu mwaka wa 1946.

Idadi ndogo ya faili zilizotolewa na makanisa ya maeneo tofauti ya Ujerumani ilimaanisha kuwa huwenda idadi hiyo ilikuwa “tonya la maji katika bahari”, mchapishaji mwenza wa utafiti huo Martin Wazlawik amesema katika mkutano na waandishi wa habari.

Jumla ya makadirio ya idadi ya wahusika wa vitendo hivyo ilikuwa karibu 3,500 kati ya wachungaji na maafisa wa kanisa hilo, kulingana na utafiti ulioidhinishwa na kanisa la EKD.

Forum

XS
SM
MD
LG