Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 01:21

Utafiti: Wamarekani hawana imani na Tik Tok


Picha inayoonyesha ofisi za Tik Tok.
Picha inayoonyesha ofisi za Tik Tok.

Idadi kubwa ya raia wa Marekani wanaamini kwamba China inatumia Tik Tok kushawishi fikra za watu nchini Marekani.

Haya ni kulingana na utafiti uliofanywa na shirika la kukusanya maoni la Ipsos kwa ushirikiano na shirika la habari la Reuters.

Ukusanyaji huo wa maoni imefanyika wakati Marekani inakaribia kuchukua hatua za kuzia kabisa mtandao wa Tik Tok nchini Marekani.

Asilimia 58 ya waliohojiwa katika utafiti huo wa siku mbili wamesema kwamba China inatumia Tik Tok kushawishi fikra za Wamarekani.

Wamarekani Warepublican wanaamini sana kwamba China inatumia Tik Tok kuwashawishi Wamarekani, ikilinganishwa na Wademokrat.

Tik Tok imesema kwamba imetumia zaidi ya dola bilioni 1.5 kuimarisha usalama wa mtandao huo na kwamba haitatoa taarifa kuhusu watumiaji milioni 170 walio Marekani kwa serikali ya China.

Forum

XS
SM
MD
LG