Chama kikuu cha upinzani nchini Uganda-FDC kimesusia mkutano kati yake na Rais Yoweri Museveni.
Mkutano huo ulilenga kutafuta mbinu ambazo uongozi wa bwana Museeveni unaweza kufanya kazi na viongozi wa chama cha FDC katika jiji la Kampala baada ya chama tawala cha bwana Museveni cha NRM kukosa kupata kiongozi yeyote aliyechaguliwa katika uchaguzi wa mwezi Februari.
Mwandishi wetu wa kampala kennes Bwire anaripoti zaidi.