Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 06:16

UNICEF yaonya Israel dhidi ya kuzuia misaada kuelekea Gaza


Malori ya misaada yakiwa kwenye mji wa wa Misri Rafah yakisuburi kuvuka mpaka kuelekea Ukanda wa Gaza. March 2, 2025.
Malori ya misaada yakiwa kwenye mji wa wa Misri Rafah yakisuburi kuvuka mpaka kuelekea Ukanda wa Gaza. March 2, 2025.

Shirika la kuhudumia  watoto la Umoja wa Mataifa, UNICEF Jumatatu limeonya kuwa uamuzi wa Israel wa kuzuia upelekaji wa misaada ya kibinadamu isipokuwa maji kwenye Ukanda wa Gaza, kwa haraka utapelekea hatari kubwa kwa watoto na familia ambazo tayari zimetatizika.

“Kusitishwa kwa upelekaji wa misaada kulikotangazwa Jumapili kutaathiri pakubwa operesheni za raia,” amesema Eduoard Beigbeder, mratibu wa kieneo wa UNICEF kwa ajili ya Mashariki ya Kati na Kaskazini mwa Afrika.

“ Ni muhimu kwa sitisho la mapigano kuendelea kuwepo, pamoja na kuruhusiwa kwa upelekaji wa misaada ili tuweze kuendelea na shughuli za kibinadamu,” Beigbeder amesema. Jumapili Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema kuwa mjumbe maalum wa Marekani kwa ajili ya Mashariki ya Kati Steven Witkoff alipendekeza kuongezwa kwa muda wa sitisho la mapigano hadi Aprili 20.

Tarehe hiyo itatoa nafasi kwa mwezi mtukufu wa Ramadan pamoja na siku kuu muhimu ya Wayahudi ya Pasaka. Ndani ya kipindi hicho, Hamas wataachilia nusu ya mateka waliyoshikiliwa na kisha kuachilia waliyobaki pale sitisho la kudumu la mapigano litakapofikiwa. “ Nimekubaliana na mpango huo ingwa kufikia sasa Hamas wameukataa,” Netanyahu alisema kupitia ujumbe wa video.

Forum

XS
SM
MD
LG