Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 09:25

UNHCR yalaani mauaji ya kinyama ya mtoto kambini Uganda


Mmoja ya kambi za wakimbizi inayoendeshwa na UNHCR iliyoko eneo la Kyangwali, Uganda, iliyopigwa picha Machi 20, 2018.
Mmoja ya kambi za wakimbizi inayoendeshwa na UNHCR iliyoko eneo la Kyangwali, Uganda, iliyopigwa picha Machi 20, 2018.

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limelaani mauaji ya kinyama yaliyofanyika kwa mkimbizi mwenye umri wa miaka miwili kutoka Sudan Kusini, katika kambi ya wakimbizi ya Palabek, Wilaya ya Lamwo, Kaskazini mwa Uganda.

“Haya ni mauaji ya kutisha na kuwa hayawezi kuhalalishwa kwani ni kitendo cha kinyama cha uwendawazimu,” amesema, Joel Boutroue, Mwakilishi Mkazi wa UNHCR nchini Uganda.

“Kwa niaba ya UNHCR, ninapenda kufikisha rambirambi zetu zenye huzuni kubwa kwa familia ya mtoto aliyeuwawa.”

Kwa mujibu wa gazeti la The Monitor nchini Uganda pia amehimiza vyombo vya usalama kuhakikisha kuwa wakimbizi wanapewa ulinzi wa kutosha katika kambi hizo.

UNHCR kupitia mshirika wake Lutheran World Federation (LWF) ilisaidia gharama za maziko ya mtoto huyo aliyeuwawa Jumamosi.

Polisi nchini Uganda inaripotiwa kuwa imeanza uchunguzi kufuatia mauaji hayo. Hata hivyo mazingira na sababu zinazohusisha mauaji hayo hazijafahamika.

UNHCR imetoa wito kwa serikali ya Uganda kuwakamata wote waliohusika na mauaji hayo na kuhakikisha haki inatendeka.

XS
SM
MD
LG