Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 20, 2023 Local time: 18:23

UN: Matumizi ya dawa ya kulevya aina ya 'cocaine' yameongezeka barani Afrika


Afisa wa polisi wa kupambana na dawa za kulevya akipakia mifuko inayojaa cocaine iliyokamatwa Chinacota, Colombia, karibu na Venezuela, Machi 2, 2016

Ofisi ya Umoja wa mataifa inayopambana na dawa za kulevya na uhalifu (UNODC) inasema uzalishaji wa Cocain ulimwenguni umeongezeka kwa viwango vya juu sana katika miaka miwili iliyopita.

Katika ripoti yake mpya, UNODC inasema matumizi ya cocaine yameongezeka barani Afrika na Asia, kadhalika katika masoko yanayofahamika huko Ulaya na mabara ya Amerika.

Inasema kilimo cha Koka Amerika Kusini kiliongezeka kwa asilimia 35 kati ya 2021 na 2022. UNODC imeongeza kuwa muongo mmoja uliopita ulishuhudia vitovu vipya vya ulanguzi wa cocaine vikiibuka Afrika magharibi na Afrika ya kati.

Mkuu wa UNODC, Ghada Waly, amesema uwezekano wa soko la cocaine kupanuka barani Afrika na Asia ni jambo linaloonekana wazi na la hatari.

Facebook Forum

XS
SM
MD
LG