Baada ya mazungumzo ya usiku mzima wakati wa kikao chao cha siku mbili mjini Brussells, nchi wanachama 27 za umoja wa ulaya leo zimeidhinisha pendekezo la tume ya utendaji ya umoja wa ulaya, kuzingatia lengo mbadala la umoja huo kwa kufikia viwango vya hewa safi ifikapo nusu karne.
Hayo ni baada ya nchi ambazo zinategemea sana mkaa wa mawe kuunga mkono lengo hilo lililoboreshwa.
Miaka mitano baada ya mkataba wa mjini Paris kuhusu hali ya hewa, Umoja wa Ulaya umesema unataka kuongoza katika vita dhidi ya viwango vya juu vya joto duniani.
Viongozi hao wamefanikiwa pia kufikia makubaliano juu ya bajeti yao na masaada wa kupambana na janga na virusi vya corona katika nchi zao.
-Imetayarishwa na Patrick Nduwimana, VOA, washington DC