Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 23, 2025 Local time: 23:20

Umoja wa Mataifa unasema muda unapita wa kuzuia janga la kibinadamu Gaza kutokea


Watoto walojeruhiwa na kuletwa hospitali mjini Gaza City
Watoto walojeruhiwa na kuletwa hospitali mjini Gaza City

Ujumbe wa waatalamu wa haki za binadam wa Umoja wa Mataifa pamoja na mfuatiliaji maalum wa Umoja wa Mataifa kwenye maeneo yanayokaliwa ya Wapalestina Francesca Albanese, umesema Alhamisi kwamba muda unapita kuweza kuzuia mauwaji ya kimbari na janga la kibinadamu kutokea huko Gaza.

Israel inasema matamshi hayo ni propaganda ya kundi la Hamas.

Katika taarifa ya pamoja waatalamu hao wanasema wana imani kwamba watu wa Palestina wako katika hatari kubwa ya mauwaji ya kimbari.

Wameongeza kusema kwamba washirika wa Israel pia wanabeba mzigo wa kuwajibika na ni lazima wachukuwe hatua za haraka na dharura sasa hivi kuzuia janga hilo kukamilika.

Mtu amekaa kwenye kifusi na kuwaza akiangalia uharibifu mkubwa wa majengo ulofanywa na jeshi la Israel kwenye kambi ya Jabaliya
Mtu amekaa kwenye kifusi na kuwaza akiangalia uharibifu mkubwa wa majengo ulofanywa na jeshi la Israel kwenye kambi ya Jabaliya

Waatalamu hao wanasema hali huko Gaza imefikia kilele cha janga kubwa, wakionya juu ya upungufu mkubwa wa maji, chakula dawa, mafuta na vifaa muhimu vya msingi pamoja na hatari ya milipuko ya ugonjwa.

Ujumbe huo wa watalaamu wa haki za binadam wanatoa kusitishwa na mashambulizi ili kuruhusu msaada wa dharura uweze kuingia kwenye ukanda huo.

Israel imedondosha mabomu makubwa na mengi kwenye ukanda wa Gaza baada ya wanamgambo wa Hamas kufanya shambulio la kipekee kuwahi kutokea mwezi uliyopita.

Forum

XS
SM
MD
LG