Mchakato wa kisiasa wa kutatua mzozo wa zaidi ya muongo mmoja nchini Libya umekwama toka uchaguzi uliopangwa kufanyika Disemba 2021 kushindikana huku kukiwa na mizozo kuhusu uhalali wa wagombea wakuu.
Kamati mpya ya wataalam wa Libya itaangalia njia za kukabiliana na masuala ambayo hayajakamilika katika sheria za uchaguzi, kaimu mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa (UNSMIL), Stephanie Koury, amesema katika taarifa yake ya video.
Alisema pia watatafuta njia za kufikia uchaguzi katika muda mfupi iwezekanavyo ikiwa ni pamoja na dhamana na muda uliopendekezwa.
Forum