Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 01:44

Ukraine yasema imetungua makombora 29 ya Russia ya masafa marefu kati ya 30


Makombora ya masafa marefu yaliyorushwa na Russia yakilenga maeneo kadhaa Ukraine.
Makombora ya masafa marefu yaliyorushwa na Russia yakilenga maeneo kadhaa Ukraine.

Russia imefyatua makombora 30 katika maeneo tofauti ya ukraine mapema Alhamisi ikiwa ni jaribio la karibuni kabisa kutokea katika jaribio la usiku la ulinzi wa anga la ukraine ambapo ilitungua 29 kati yake maafisa wamesema.

Mtu mmoja amekufa na wengine wawili wamejeruhiwa na makombora ya Russia ambayo yamepita na kupiga katika jengo la kiwanda kusini mwa mji wa Odesa , hiyo ni kwa mujibu wa Serhiy Bratchuk , msemaji wa utawala wa kijeshi wa eneo hilo.

Licha ya mashambulizi ya anga ya Russia , China imesema mjumbe wake maalumu alikutana na rais Volodymir Zelensky wakati wa mazungumzo huko Kyiv mapema wiki hii na mwanadiplomasia mkuu wa ukraine.

Msemaji Wang Wenbin alisema alhamisi kwamba pande zinazogombana inabidi ziwe katika hali ya kuaminiana ili hatua za maendeleo zipigwe.

Ofisi ya rais wa ukraine imesema , maafisa wa nchi hiyo wakati wa mazungumzo walitaka kupata uungwaji mkono wa China kwa ajili ya kuisaidia Kyiv katika mpango wa amani. Pendekezo la zelensky ni pamoja na kurejeshwa kwa uadilifu wa eneo la nchi yake, kuondolewa vikosi vya Russia na kumuwajibisha rais wa Russia Vladmir Putin kisheria kutokana na uvamizi wa february 2022.

XS
SM
MD
LG