Oleh Kiper, Gavana wa Odesa, amesema shambulizi lilipiga eneo la Izmail kwa mara ya nne ndani ya siku tano na kumjeruhi mtu mmoja.
Ameongeza kusema pia shambulizi liliharibu miundombinu ya bandari, na jengo la utawala. Wizara ya ulinzi ya Russia imesema imeharibu ndege mbili zisizokuwa na rubani za Ukraine katika mkoa wa Rostov pamoja na Bryansk, na nyingine katika vitongoji vya Moscow.
Meya wa Moscow, Sergei Sobyanin amesema kupitia Telegragram kwamba mabaki ya ndege isiyo na rubani iliyotunguliwa yaliangukia katika wilaya ya Ramensky na hayakufanya uharibifu ama kusababisha vifo.
Forum