Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 16:17

Ukraine: Kundi la nchi tajiri zenye demokrasia G7 zatoa ahadi kuungana dhidi ya vita vya kichozi vya Russia


Mawaziri wa Mambo ya Nje na maafisa wa G7 wakiwa katika utekelezaji wa majukumu yao pamoja na kupata chakula cha usiku kwenye mkutano wa kundi la G7 Japan, Aprili 16, 2023. Picha kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Japan/ kupitia REUTERS
Mawaziri wa Mambo ya Nje na maafisa wa G7 wakiwa katika utekelezaji wa majukumu yao pamoja na kupata chakula cha usiku kwenye mkutano wa kundi la G7 Japan, Aprili 16, 2023. Picha kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Japan/ kupitia REUTERS

Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan Yoshimasa Hayashi amesema Jumanne kundi la nchi tajiri duniani zenye demokrasia  G7 zimeahidi kuungana pamoja dhidi ya  vita vya kichokozi vya Russia vya uvamizi wa Ukraine.

Waziri huyo amesema hayo wakati wa kufunga mkutano wao wa G7 na kueleza kuwa walikuwa na nia ya dhati kuinua na kuweka vikwazo dhidi ya Moscow.

Wakizungumzia kuhusu China, Hayashi alisema mawaziri wa G-7 walisisitiza umuhimu wa kufanya mazungumzo ya wazi na kuwasilisha wasiwasi wao moja kwa moja.”

Hayashi alisisitiza umuhimu wa kuwa na amani na uthabiti nchini Taiwan na kusema kuwa mawaziri wa mambo ya nje katika mkutano huo wameapa kuendelea na juhudi za kidiplomasia.

Viongozi na mawaziri wa mambo ya nje wa G-7 hasa Ufaransa na Ujerumani hivi karibuni waliitembelea China na kumekuwa na wasiwasi mkubwa unaokua baada ya Beijing hivi karibuni kutuma ndege za kivita na meli kuzingira Taiwan.

Beijing imekuwa ikiongeza kwa kasi silaha za nyuklia na kuchukua msimamo mkali zaidi kwa madai yake katika South China sea na kutengeneza mazingira ya uchokozi.

XS
SM
MD
LG