Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 03, 2024 Local time: 02:48

Japan: Mawaziri wa mazingira wa G7 wanajadili nishati mbadala kuimarisha usalama wa kiuchumi


Gari la Umeme likijaza charji katika kituo cha magari ya umeme Los Angeles, 17 Oct. 2018.
Gari la Umeme likijaza charji katika kituo cha magari ya umeme Los Angeles, 17 Oct. 2018.

Mawaziri wa mazingira kutoka kundi la G7 wanakutana Ijumaa Sapporo  kaskazini mwa Japan,  hatua iliyopelekea kuwepo ulinzi  wa hali ya juu kwenye eneo la Mkutano.

Washiriki wa G7 wanatarajiwa kufanya Mkutano wa mabadiliko ya hali ya hewa ambao wataomba hatua zaidi zichukuliwe katika muongo muhimu lakini pia kueleza bayana kuhusu migawanyiko juu ya ahadi kubwa za mafuta yatokanayo na nishati mbali mbali.

Waziri wa viwanda wa Japan Yasutoshi Nishimura anafikiria kupendekeza mpango wa madini muhimu kwa betri za magari ya umeme na betri katika juhudi za kuimarisha usalama wa kiuchumi, Yomiuri ameripoti.

Nchi zinatarajiwa kujumuisha mipango kwa ajili ya kuboresha mahitaji muhimu ya muda mrefu na usambazaji wa cobalt, lithiamu na nikeli, pamoja na kuunda mfumo mzuri wa utekelezaji wa mpango huo, taarifa ya maandishi imesema.

Pia watatoa zaidi ya yen trillion moja ambazo ni sawa na dola bilioni 7.55 kwa msaada wa kifedha kwa maendeleo ya madini.

Nchi hizo pia zinatarajiwa kukubaliana na kanuni za kimsingi za kufanya biashara ya kupunguza utoaji wa gesi chafu .

XS
SM
MD
LG