“Mwaka mmoja uliopita, dunia ilikuwa inaamini kwamba Kyiv itaanguka, Biden aliuambia umati wa zaidi ya Wapoland 10,000 waliokusanyika nje katika Jengo la Royal Castle.
“Kweli, nimetoka hivi punde kutembelea mji wa Kyiv, na ninaweza kuripoti kuwa Kyiv inasimama imara. Inasimama imara, na muhimu zaidi, inasimama huru.”
Biden ameahidi kwamba msaada kwa Ukraine hautasitishwa na NATO haitagawanyika.
“Ukraine kamwe haitashindwa na Russia,” alitangaza, akisema muungano huo una dhamira zaidi kuliko hapo awali, ya kuipa Ukraine zana na misaada ya kibinadamu kuisaidia kujihami dhidi ya Russia.
Facebook Forum