Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 06:26

Uingereza yajikita kuwa mstari wa mbele kushughulikia mzozo wa Ukraine na Russia


Uingereza, Ufaransa na Ukraine zimekubaliana kufanyia kazi mpango wa kusitisha mapigano kuwasilishwa kwa Marekani, Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, amesema Jumapili alipokuwa akijiandaa kuwa mwenyeji wa mkutano wa viongozi wa Ulaya kujadili kumaliza vita.

Mkutano huo umegubikwa na kuzomewa vikali kwa rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, na Rais wa Marekani, Donald Trump, kwa “kutoshukuru uungwaji mkono wa Marekani” katika vita vya Ukraine dhidi ya uvamizi wa Russia, wakati walipokutana Ijumaa katika White House.

Lakini Waziri Mkuu Starmer, amesema analenga kuwa daraja la kurejesha mazungumzo ya amani na alitumia kuvunjika kwa mazungumzo hayo kama fursa ya kuungana tena na Marais Trump na Zelenskyy pamoja na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron badala ya kuongeza mvutano.

Forum

XS
SM
MD
LG