Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 16, 2025 Local time: 19:32

Uingereza yadai Russia ilihifadhi mabombora ya anga ya majira ya baridi


Wizara ya Ulinzi ya Uingereza, Jumapili imesema katika taarifa yake ya kila siku ya kijasusi kuhusu Ukraine, kwamba Russia, imekuwa ikihifadhi makombora ya anga au ALCM kwa ajili ya matumizi katika kampeni yake ya majira ya baridi kali dhidi ya Ukraine.

Makombora hayo yalitumiwa Desemba 7, wizara hiyo imesema katika wimbi kubwa la mashambulizi yaliyoilenga Kyiv, na Ukraine, ya kati.

Wakati wizara ya Uingereza inasema kurushwa kwa makombora hayo mwezi Desemba huenda kulilenga kuharibu miundombinu ya nishati ya Ukraine, na ripoti za awali zinaonyesha kuwa Ukraine ilifanikiwa kuyazuia.

Uharibifu kutoka kwa makombora hayo ulikuwa mdogo kwa mujibu wa ripoti ya Uingereza, licha ya kuuwawa kwa raia mmoja katika mashambulizi.

Wakati huo huo, Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy, anafanya safari yake ya kwanza Amerika Kusini, alitarajiwa kuhudhuria kuapishwa kwa Javier Milei, kuwa rais mpya wa Argentina.

Forum

XS
SM
MD
LG