Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:58

Uingereza kuongeza kodi na kubana matumizi kutokana na mfumuko wa bei


Waziri mkuu wa Uingereza Rishi Sunak akiwa nje ya ofisi yake iliyo barabara ya Downing, London, Uingereza, Oct. 26, 2022.
Waziri mkuu wa Uingereza Rishi Sunak akiwa nje ya ofisi yake iliyo barabara ya Downing, London, Uingereza, Oct. 26, 2022.

Waziri wa fedha wa Uingereza Jeremy Hunt amesema kwamba anapanga kuongeza kodi na kupunguza matumizi ya serikali, ili kuwaonyesha raia wa Uingereza kwamba nchi hiyo inaweza kusimamia vyema uchumi wake baada ya kuyumba yumba kwa masoko ya fedha, na kupelekea kujiuzulu kwa Liz Truss kama waziri mkuu.

Hunt hata hivyo amesema kwamba kaya maskini hazitaongezewa kodi na kwamba hatua ya kupunguza matumizi kwa huduma za umma yatakuwa na uwiano.

Akizungumza kabla ya kutangaza mipango ya bajeti ya serikali siku ya alhamisi, Hunt alisema hakutaka kuzungumzia hali inayotarajiwa ya kudorora kwa uchumi, lakini amesema kwamba atapunguza nakisi ya bajeti ambayo imeongezeka tangu kutokea kwa janga la virusi vya Corona, na uvamizi wa kijeshi wa Russia nchini Ukraine.

Hunt na waziri mkuu Rishi Sunak wameonya kwamba watachukua maamuzi magumu sana, ili kukabiliana na mfumuko wa bei ambao umefikia asilimia 10.

Wabunge wengi wa chama kinachotawala cha Conservative wanapinga nyongeza ya kodi na huenda hatua ya serikali ya Sunak kuongeza kodi ikasababisha tena mpasuko ndani ya chama hicho.

XS
SM
MD
LG