Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya leo amefanya ziara ya siku moja mjini Juba, Sudan Kusini, ambako amekutana na Rais Salva Kiir katika Ikulu ya nchi hiyo, na kumshinikiza atekeleze makubaliano ya kutafuta amani yaliyotiwa saini mapema mwaka huu.
Katika taarifa iliyotolewa na ikulu ya Nairobi, Kenyatta aidha amechukua nafasi hiyo kumwelezea Kiir kwamba eneo la Afrika Mashariki na Kati linamuunga mkono katika juhudi zake za kutafuta amani.
Kutadhmini hayo, BMJ Muriithi alizungumza na naibu wa msemaji wa ikulu, Munira Mohamed, na kwanza akamuuliza ni upi hasa umuhimu wa ziara hiyo iliyofanywa na rais Kenyatta mjini Juba: