Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Februari 12, 2025 Local time: 08:26

Uhispania yanyakua ubingwa wa kombe la dunia la wanawake


Wachezaji wa Uhispania wakisherekea ubingwa katika fainali ya kombe la dunia la wanawake kwenye uwanja wa michezo wa mjini Sydney, Australia, Agosti 23.
Wachezaji wa Uhispania wakisherekea ubingwa katika fainali ya kombe la dunia la wanawake kwenye uwanja wa michezo wa mjini Sydney, Australia, Agosti 23.

FIFA WOMEN’S WORLD CUP FINAL Uhispania imeishinda Uingereza katika fainali ya kombe la dunia la wanawake leo Jumapili kwa kuifunga bao 1 kwa sifuri na kuhitimisha mashindano ambayo yamevunja rekodi kwa kuhudhuriwa na kutazamwa na watu wengi sana kupitia televisheni.

Australia na New Zealand, walikuwa wenyeji wa michuano hiyo, lilikuwa kombe la dunia la wanawake la tisa na la kwanza kufanyika katika kanda ya kusini.

Licha ya mashabiki kutokuwa na hamu ya kufika uwanjani baada ya Australia kuondolewa katika duru ya nusu fainali, watu wasiopungua milioni 2 walifika uwanjani katika miji tisa wenyeji wa michezo hiyo, na zaidi ya watu 75,000 walihudhuria fainali ya leo Jumapili.

Maelfu ya mashabiki walimiminika karibu na uwanja wa michezo wa Australia mjini Sydney saa chache kabla ya kuanza kwa mchezo wa fainali Jumapili.

Forum

XS
SM
MD
LG