Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 09, 2025 Local time: 10:34

Ufaransa yaanza kuwaondoa raia wake nchini Niger


Raia wa Ufaransa wakusanyika kwenye uwanja wa ndege wa mjini Niamey nchini Niger, wakisubiri kurudishwa nchini mwao na ndege ya kijeshi, Agosti 1, 2023
Raia wa Ufaransa wakusanyika kwenye uwanja wa ndege wa mjini Niamey nchini Niger, wakisubiri kurudishwa nchini mwao na ndege ya kijeshi, Agosti 1, 2023

Ndege ya kwanza kati ya tatu za kuwaondoa raia wa Ufaransa na Ulaya nchini Niger iliondoka Jumanne jioni, siku sita baada ya mapinduzi ya kijeshi yaliyomuondoa madarakani mmoja wa viongozi wa mwisho anayeungwa mkono na nchi za magharibi katika eneo la Sahel.

Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Catherine Colonna aliiambia AFP “ Kuna watu 262 ndani ya ndege hiyo aina ya Airbus 330, wakiwemo zaidi ya watoto wachanga 10.”

Colonna alisema ndege hiyo ilitarajiwa kutua kwenye uwanja wa ndege wa Paris Roissy Charles de Gaulle nyakati za usiku.

Yakiwa mapinduzi ya kijeshi ya tatu katika eneo hilo, Rais wa Niger Mohamed Bazoum aliondolewa madarakani na walinzi wake, hali ambayo ilizusha wasiwasi nchini Ufaransa, mtawala wa zamani wa kikoloni wa Niger na mshirika wake wa muda mrefu.

Baada ya umati wa watu wanaoipinga Ufaransa kukusanyika siku ya Jumapili nje ya ubalozi wa Ufaransa na Niger kuishtumu Ufaransa kupanga njama ya kuingilia kati kijeshi, Paris ilisema Jumanne kwamba itawaondoa raia wake na kusaidia kuwaondoa raia wa Ulaya pia.

Forum

XS
SM
MD
LG