Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 08, 2025 Local time: 20:22

Uchunguzi unaendelea kuhusu ajali ya ndege Marekani


Mabaki ya ndege yakitolewa kwenye mto Potamic karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Ronald Reagan Washington , Jan. 30, 2025.
Mabaki ya ndege yakitolewa kwenye mto Potamic karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Ronald Reagan Washington , Jan. 30, 2025.

Waokoaji wanaendelea kutoa mabaki ya ndege mbili zilizogongana angani na kusababisha vifo vya watu 67 karibu na mji mkuu wa Marekani Washington DC, jumatano usiku.

Wachunguzi kutoka taasisi tofauti za Marekani wamepata kisanduku kinachonasa mawasiliano kati ya rubani na waelekezi wa ndege kinachojulikana kama Black Box, kutoka kwenye ndege ya shirika la American, ambayo ilivunjika katika vipande kadhaa na kuanguka katika mto Potamac, baada ya kugongana na helikopta ya kijeshi ya Marekani.

Bodi ya taifa inayosimamia usalama wa safari itakusanya taarifa kutoka kwenye vifaa vya kunasa mawasiliano vya ndege hiyo ili kubaini kilichopelekea ajali hiyo.

Hakuna mtu aliyenusurika katika ajali hiyo iliyotokea karibu na uwanja wa ndege wa kitaifa wa Ronald Reagan.

Kuna ripoti kwamba kulikuwa hakuna wafanyakazi wa kutosha kuelekeza ndege wakati wa ajali hiyo na kwamba mtu mmoja alikuwa anafanya kazi ya watu wawili.

Forum

XS
SM
MD
LG